Mara nyingi, tumesikia hadithi nyingi kuhusu wafu, wengine wakiamini kuwa mtu anapokufa huwa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine, je! Ukweli halisi ni upi??
Karibu tujifunze pamojaa kwa kuangalia maandiko yanasemaje!!
MWANADAMU ALIUMBWA
Mwanadamu ni matokeo ya udongo jumlisha pumzi ya uhai,
[Mwanadamu=udongo+pumzi ya uhai]
BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo:2:7)
Hivyo, ukichukua udongo ukatoa na pumzi ya uhai unapata maiti,
[Maiti=Udongo-pumzi ya uhai]
KIFO HAUKUWA MPANGO WA MUNGU
Kifo ni matokeo ya dhambi, baada ya adamu na Hawa kuvunja sheria ya Mungu, pale kwenye bustani ya Edeni[mwanzo 3:1-24]
Ikiwa Kama adamu na Hawa wasingetilia Shaka maagizo ya Mungu, Leo kifo kisingekuwepo kabisaa hakuna hata mmoja ambaye angekuwa anahisi maumivu tunayohisi leoo.... (EGW, Pendo lisilo kifani, sura ya Anguko la Mwanadamu)
Biblia inafananisha KIFO na usingizi, maana baada ya muda Yesu akirudi atawafufua watu wote....ni usingizi ambaye aliyelaa hawezi kujiamusha/kuamshwa, Wala hauna ndoto [Yohana 5:28]
WALIOKUFA WAKO WAPI HASA?
Agano la Kale linapaita mahali walipo wafu kuwa ni sheol (Kiebrania) na Agano Jipya hades (Kigiriki).
Katika Maandiko, maana rahisi ya sheol (kuzimu) ni kaburi. Maana ya hades ni sawa na maana ya sheol.
Wafu wote huenda mahali hapo(Zab.89:48), wema kwa waovu.
Yakobo alisema atamshukia mwanawe hata kuzimu (Mwa.37:35).
Ardhi ilipofunguka, iliwameza Kora pamoja na wenzake hadi kwenye sheol (Hes.16:30).
1. Aliyekufa hajui neno lolote
Kwa mujibu wa maandiko, wale wanaoamini kuwa maiti huwa anaweza kuhisi maumivu, Kama sisi tulio hai.... Wanakosea!
Mhubiri 9:5
[5]kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa.
2. Katika usingizi huo, hakuna kufikiri, au kutenda Kama aliye hai.
Kwa kuwa mawazo yake hupotea, hawezi kufikiri chochote! (Zab.146:4), (Qurani 12:106 ufafanuzi), Quran 35:22
3. Aliyekufa hawezi kutokea Kama muzimu, au Kama roho
Ikiwa aliyekufa hajui chochote je, mbona Mara nyingi tumetokewa na bibi, babu, ndugu, jamaa na marafiki kwenye ndoto hao ni akina Nani Kama wafu hawawezi kuzungumza nasi?
Jibu: 2 Wakorintho 11:14.
“Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.”
Anayekuja katika usingizi ....huwa sio Yeye maana aliyekufa hawezi ongea, Ila ni SHETANI anajigeuza na kuvaa uhusika wa rafiki, ndugu yako! Ili apate kukudanganya!....
Amewahi kufanya hivyo, ili kudanganya mfalme wa Israel, [1 Samweli 28:7–25]
YESU AKIJA ATAWAFUFUA WAFU WOTE!
Biblia inasema:
Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele. (Daniel 12:2)
Hii inamanisha watakatifu na waovu wote...wako kaburini, YESU akija atawafufua kila mmoja alipwe sawa sawa na matendo yake!!
.............................................................................
UKIMTUMAINI, UKIMWAMINI, NA KUMFATA YESU, UZIMA WA MILELE NI WAKO!
Wanaomtumaini Yesu, hata wanapokufa wanakufa katika TUMAINI la kufufuliwa na kupata uzima wa milele...
Yohana 6:39-40
[39]Na mapenzi yake aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika wote alionipa nisimpoteze hata mmoja, bali nimfufue siku ya mwisho.
[40]Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.
Barikiwa Sana....
Amani ya Bwana iwe juu yako.. Hesabu 6:25
Comments
Post a Comment