Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2025

ANGUKO LA MWANADAMU

 Katika somo la UUMBAJI, tuliona kuwa Mungu aliumba dunia ikiwa nzuri, yenye kuvutia Sana!  Swali ni ikiwa hivi ndivyo, shida ilitokea wapi...? Maana Leo dunia imejaa magonjwa, huzuni, vilio, vifo, shida ilianzia EDENI,  ADAM & HAWA EDENI  Mwanzo 2:8-9, 2:16-17  [8]BWANA Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya [9]BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.  [16]BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula  [17]walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.  ------  MTI WA UJUZI WA MEMA & MABAYA KAMA KIPIMO CHA UTII  Katika kitabu Cha Ellen G White, Pendo lisilo kifani sura isemayo msiba, anasema!.  ------- .....Mungu alichagua kuujaribu uaminifu...

ANGUKO LA LUSIFA

 Mwandishi mmoja (Ellen G White)  katika kitabu chake Cha Pendo lisilo kifani(PLK) sura isemayo Uasi, anaandika maneno yafuatayo! Lusifa alikuwa malaika mkuu Kabla ya uasi wake mbinguni, Lusifa alikuwa malaika mkuu na aliyetukuka, ambaye kwa heshima, alikuwa akimfuatia Mwana wa Mungu(Yesu Kristo)  Uso wake, kama zilivyokuwa za malaika wengine, ulikuwa ni wa upole ulioangaza furaha. Kipaji cha uso wake kilikuwa kimeinuka na kipana, kikionesha uwezo mkubwa wa kiakili...... Nuru ya pekee ilimulika kutoka katika uso wake ikiangaza kumzunguka kwa uangavu na uzuri kuliko ilivyokuwa kwa malaika wengine [EGW, PLK 5.1]  Uzuri wake lusifa, ulimfanya awe na kiburi Mungu alikuwa amempa cheo cha juu, lakini hilo halikumfanya arejeshe shukrani na sifa kwa Muumba wake.  Alitamani kufikia kimo cha Mungu mwenyewe.... Aliona fahari kwa sababu ya hadhi yake iliyotukuka. Alijua kuwa alikuwa anaheshimiwa na malaika.... Alikuwa amepata fursa ya kuwa karibu na Muumbaji mkuu, na miale ...