Mwandishi mmoja (Ellen G White) katika kitabu chake Cha Pendo lisilo kifani(PLK) sura isemayo Uasi, anaandika maneno yafuatayo!
Lusifa alikuwa malaika mkuu
Kabla ya uasi wake mbinguni, Lusifa alikuwa malaika mkuu na aliyetukuka, ambaye kwa heshima, alikuwa akimfuatia Mwana wa Mungu(Yesu Kristo)
Uso wake, kama zilivyokuwa za malaika wengine, ulikuwa ni wa upole ulioangaza furaha. Kipaji cha uso wake kilikuwa kimeinuka na kipana, kikionesha uwezo mkubwa wa kiakili......
Nuru ya pekee ilimulika kutoka katika uso wake ikiangaza kumzunguka kwa uangavu na uzuri kuliko ilivyokuwa kwa malaika wengine [EGW, PLK 5.1]
Uzuri wake lusifa, ulimfanya awe na kiburi
Mungu alikuwa amempa cheo cha juu, lakini hilo halikumfanya arejeshe shukrani na sifa kwa Muumba wake.
Alitamani kufikia kimo cha Mungu mwenyewe....
Aliona fahari kwa sababu ya hadhi yake iliyotukuka. Alijua kuwa alikuwa anaheshimiwa na malaika....
Alikuwa amepata fursa ya kuwa karibu na Muumbaji mkuu, na miale ya daima ya nuru tukufu iliyomzunguka Mungu wa milele kwa namna ya pekee iliangaza juu yake.
Alifikiria jinsi ambavyo malaika walitii amri zake kwa haraka na furaha. Je mavazi yake hayakuwa nuru na ya kupendeza? Kwa nini Kristo(Yesu) aheshimiwe kiasi kile badala yake? - EGW, PLK 5.2
_-_-_-_-_-_-_-
BWANA alimuumba lusifa kwa namna ya ajabu Sana, maana aliumbwa kwa Vito vya thamani.. akiki, yakuti manjano, almasi, n.k [Ezekiel 28:13]
Lusifa aliangusha jeshi kubwa la malaika
Kwa sababu ya uzuri wake, akaanza kutamani nafasi ya Mungu, BWANA alimpatia nafasi ya kutubu lakini, hakuitumia vizuri, taratibu akawashawishi ¹/3 ya jeshi la malaika wa mbinguni wakawa upande wake, hao ndo wanaitwa leo (Mapepo na Majini) akawaahidi kuwa baada ya kumpindua Mungu, atatengeneza serikali Bora kuliko ya Mungu, ambayo kwayo kila mmoja ataweza kufanya atakavyo!
Lusifa kuondolewa mbinguni
Kwakuwa Yeye lusifa ni kiumbe, kamwe asingeweza kumpindua Mungu, BWANA kwa upendo wake alivyoona Lusifa hajafanya Toba ya dhati akaamua kumfukuza Yeye na jeshi lake watoke mbinguni....ili kila mmoja aone uovu uliokuwa umefichika ndani yake, ndo maana hakumwangamiza kwa muda huo... [Ezekiel 23:17], pia Soma [Ufunuo 12:7-9]
Shetani alipoondolewa mbinguni, aliwatuma malaika wake wakaangalie katika sayari zingine ikiwa itapatikana nafsi waingie, Ila walikosa katika sayari zingine.....mwisho wa siku wakabahatika kupata nafasi katika sayari hii ya dunia.
_-_-_-_-_-_-_-_-_--_-_-_-_-_-_--_-_-_-_-_-_-_-_--_-_-_
Toka lusifa Hadi kuitwa Shetani
Kuanzia hapo jina lake likabadilika kutoka kuitwa LUSIFA(Nyota ya Asubuhi) mbeba Nuru Hadi kuitwa SHETANI, IBILIS (Mshitaki, mpinzani, au adui) EGW, PLK 7.3
Hadi leo shetani Yupo, na Hukumu yake ni kuangamizwa kwa Moto wa milele Siku ya Hukumu ikifika, Hana nafasi ya kutubu Tena!! Anachokifanya ni kukusanya wafuasi ili Siku ya mwisho apotee na idadi kubwa!!
====================================
Ila usiogope, Mungu ameweka nafasi ya kukuokoa! Ikiwa unatamani kukwepa adui huyu mkuu....
Karibu SoMo linalofuata [Anguko la Mwanadamu]
----Amani ya Bwana iwe Juu yako--- Hesabu 6:25
Comments
Post a Comment