Skip to main content

ANGUKO LA MWANADAMU

 Katika somo la UUMBAJI, tuliona kuwa Mungu aliumba dunia ikiwa nzuri, yenye kuvutia Sana! 

Swali ni ikiwa hivi ndivyo, shida ilitokea wapi...? Maana Leo dunia imejaa magonjwa, huzuni, vilio, vifo, shida ilianzia EDENI, 


ADAM & HAWA EDENI 

Mwanzo 2:8-9, 2:16-17 

[8]BWANA Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya

[9]BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya. 

[16]BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula 

[17]walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika. 

------ 

MTI WA UJUZI WA MEMA & MABAYA KAMA KIPIMO CHA UTII 

Katika kitabu Cha Ellen G White, Pendo lisilo kifani sura isemayo msiba, anasema!. 
-------
.....Mungu alichagua kuujaribu uaminifu wao kabla hajawafanya kuwa salama milele. Shetani aliruhusiwa kuwajaribu. Iwapo wangelishinda jaribu lile, wangepata kibali cha Mungu na malaika wa mbinguni milele zote. - PLK 14.2

----Mungu, alitaka kupima uaminifu wao, Shetani alikuja kwa Umbo la nyoka, Kisha  hichi ndicho alicho fanya!!---

HAWA ALIDANGANYWA 

Mwanzo 3:1-4
[1]Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya BWANA Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani? 
[2]Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; 
[3]lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. 
[4]Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa! 
===============================

Shetani katika Umbo la nyoka, akisha kumshawishi, Hawa! Kwa huzuni, Hawa akashawishika! ✍️

Biblia inasema: 
Mwanzo 3:6
[6]Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala. 

HUKUMU YA MUNGU EDENI 

Baada ya wawili Hawa, kutilia Shaka maagizo ya Mungu na kufuata uongo wa shetani, wakawa wamevunja Sheria ya YEHOVA!! 
Mungu alipowatembelea kuwatafuta(ilikuwa kawaida ya MUNGU kuwatembelea) wakaanza, kujificha! akisha kuhojiana nao, akahitimisha kwa kuilaani ardhi, nyoka, na kuwatangazia madhara yatakayowapata baada ya kuvunja agizo lake! [Mwanzo 3:8-19] 
-----------------------------------------------

Kuanzia hapo dhambi ikaingia, kifo kikaingia, magonjwa, shida, mateso! Mwanadamu akawa ameanguka! Kwa kuvunja maagizo ya Mungu!! ✍️
=============
Pamoja na Adam na Hawa kuvunja maagizo ya Mungu, Mungu aliandaa mpango wa kuwatoa katika shimo la dhambi, SoMo linalofuata! Tutajifunza Juu suluhisho baada ya Anguko....... 

----Amani ya Bwana iwe Juu yako---.                  Hesabu 6:25. 


Comments

Popular posts from this blog

MTU ANAPOKUFA ANAENDA WAPI?

Mara nyingi, tumesikia hadithi nyingi kuhusu wafu, wengine wakiamini kuwa mtu anapokufa huwa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine, je! Ukweli halisi ni upi??  Karibu tujifunze pamojaa kwa kuangalia maandiko yanasemaje!!  MWANADAMU ALIUMBWA Mwanadamu ni matokeo ya udongo jumlisha pumzi ya uhai,  [Mwanadamu=udongo+pumzi ya uhai] BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo:2:7) Hivyo, ukichukua udongo ukatoa na pumzi ya uhai unapata maiti,  [Maiti=Udongo-pumzi ya uhai] KIFO HAUKUWA MPANGO WA MUNGU Kifo ni matokeo ya dhambi, baada ya adamu na Hawa kuvunja sheria ya Mungu, pale kwenye bustani ya Edeni[mwanzo 3:1-24] Ikiwa Kama adamu na Hawa wasingetilia Shaka maagizo ya Mungu, Leo kifo kisingekuwepo kabisaa hakuna hata mmoja ambaye angekuwa anahisi maumivu tunayohisi leoo.... (EGW, Pendo lisilo kifani, sura ya Anguko la Mwanadamu) Biblia inafananisha KIFO na usingizi, maana baada ya muda Yesu akirudi...

UHALISIA WA UWEPO WA MUNGU

 JE MUNGU YUPO KWELI?  Watu wengi wamehoji maswali Mengi ikiwa Mungu yupo au la, na baadhi wamefikia hatua ya kusema kuwa hakuna Mungu!  Swali linakuja ikiwa Mungu yupo wawezaje kuthibitisha Imani yako?  UTHIBITISHO WA  UWEPO WA MUNGU  Mungu, yupo! Upo uthibitisho tosha kujibu swali hili Kama ifuatavyo!.  1. Uwepo wa Ulimwengu huu  Vitu vinavyoonekana vyote, Kama vile mimea, wanyama, mfumo wa jua (Solar system) na sayari zingine zote, kuwepo kwake Lazima awepo mwasisi wake! Maana hakuna uthibitisho wowote unaonesha kuwa sayari yaweza jiumba yenyewe!!, Wala dhana ya uibukaji haileti mantiki kusema mfumo wa Jua ulivyokaa uliibuka tuu.  2.  Mpangilio, mwafaka na Muundo wa Ulimwengu.  Jinsi Ulimwengu ulivyo, Kuna aliyepangilia, aka design(Muundo) ili kupata rangi/mwonekano mzuri wenye kuvutia, angalia aina za mimea, maua, wanyama tofauti kwa aina zake, ndege tofauti wakivutia sana!  Jua litoke mashariki kwenda magharibi Bila kuhama...

SIKU YA SABATO NI IPI?

Wengi, wanatunza Siku ya jumapili na wengine Siku ya jumamosi... Swali linakuja je, Kati ya hizi mbili ipi ni Siku ya kweli?...  SABATO YA BWANA  Biblia inasema;  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. [Waefeso 4:5] Kwa mujibu wa Biblia upo ubatizo mmoja(wa maji Mengi) Yuko Mungu mmoja na Imani moja.....(Siku ya ibada lazima iwe moja) Kama wakiwa na Imani moja....  SABATO NI AMRI YA NNE Katika kutoka 20:8-11 tunasoma maneno haya;  [8]Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.  [9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;  [10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.  [11]Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.  -----------------------------...