Skip to main content

KUZALIWA MARA YA PILI

SoMo lililopita tuliona kuwa ukimwamini Yesu, ukatubu utasamehewa dhambi, hata Kama zilikuwa nyingi kiasi gani....upendo mkuu ajabu! Kiroho mtu aweza kuzaliwa Mara ya pili kwa njia ya ubatizo!...... 

Kwa njia ya ubatizo, mtu atamkiri Yesu, kuwa ni mwokozi wake, ndiyo njia Mungu aliyoiweka ya kutuvusha kutoka mahali pa dhambi, kutuunganisha na Mwokozi, kwa kufanya tendo hili...inakuwa umemkubali Yesu waziwazi.... hivyo, baada ya kubatizwa atakupokea, Kama mtoto wake!....nawe utakuwa umeanza safari mpya ya maisha! 

UBATIZO

Je, mtu anayebatizwa anapaswa awe na sifa gani? 
Biblia inasema: 
Marko 16:15-16
[15]Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. 
[16]Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. 

Kutoka kwenye Aya hii tunapata Mambo 3. 

a) Injili 

Kabla mtu hajabatizwa lazima ajue kweli (Neno la Mungu), ili aelewe anabatizwa kwa sababu gani!. 

b)Imani 

Baada ya kuhubiriwa, na kuitikia sauti ya Roho mtakatifu, ataamini ya kuwa aliyofundishwa ni kweli, hii ni hatua ya pili, hawezi amini Bila kufundishwa! 

c) Ubatizo 

Baada ya kufundishwa, na kuamini, hatua ya mwisho atafanya uamuzi wa kuyatoa maisha yake kwa mwokozi kwa njia ya ubatizo!. 

Zingatia: 

Mtoto mdogo hawezi batizwa, maana hizi hatua tatu haziendani na Yeye! Hawezi elewa, hawezi amini...mpaka akifikia umri wa kujitambuaa ndipo aweza kubatizwa!
-----------------------------------
-----------------------------------
-----------------------------------

UBATIZO SAHIHI NI UPI? 

Kuna batizo za aina nyingi hapa duniani....je, katika hizo upi ni ubatizo sahihi unaotakiwa? Ambao unakubalika mbele ya Mungu mwenyezi? 

Biblia inasema: 
Waefeso 4:5
Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja

Kwa mujibu wa Biblia ubatizo upo mmoja tuu! Nao sio mwingine ni ule alionesha Yesu kristo mwenye kuanzisha Imani yetu! 

*YESU ALIBATIZWA KWA MAJI MENGI*
Mathayo 3:13-16
[16]Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake
--------------------------

Hivyo, ubatizo sahihi unaotakiwa ni ubatizo aliobatizwa Yesu! 

Biblia inasema: 
1 Yohana 2:6
Yeye asemaye ya kuwa anakaa ndani yake, imempasa kuenenda mwenyewe vile vile kama yeye alivyoenenda 
 


Maana ya Neno Ubatizo: 
Neno Batiza ni neno la kiyunani (Baptizo) lenye maana ya *zamisha* tosa* 
Huwezi zama, ndani ya maji ya bakuri, huwezi zama ndani ya Moto, Ila ndani ya maji Mengi unaweza kuzamishwa! 

MAANA HALISI YA UBATIZO## 
Kubatizwa ndani ya maji Mengi Kama alivyo fanya mwokozi Kuna Manisha Mambo yafuatayo! 
I)Kuzika dhambi, 
II)kufa pamoja na Mwokozi
II)kufufuka pamoja na Yesu, ukiwa kiumbe kipya! 
[Warumi 6:1-4] 
=====================
=====================
=====================
Kama umetambua ya kwamba Mungu ndiye muumbaji, naye anakupenda hata kumtoa mwanae wa pekee ili usiangamie, ameweka ubatizo Kama njia ya kuwapokea wote wanaitikia upendo wake! Je, unaweza kuwa miongoni mwao?? Usiogope unaweza! 

-----Amani ya Bwana iwe Juu yako---      Hesabu 6:25 

Comments

Popular posts from this blog

MTU ANAPOKUFA ANAENDA WAPI?

Mara nyingi, tumesikia hadithi nyingi kuhusu wafu, wengine wakiamini kuwa mtu anapokufa huwa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine, je! Ukweli halisi ni upi??  Karibu tujifunze pamojaa kwa kuangalia maandiko yanasemaje!!  MWANADAMU ALIUMBWA Mwanadamu ni matokeo ya udongo jumlisha pumzi ya uhai,  [Mwanadamu=udongo+pumzi ya uhai] BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo:2:7) Hivyo, ukichukua udongo ukatoa na pumzi ya uhai unapata maiti,  [Maiti=Udongo-pumzi ya uhai] KIFO HAUKUWA MPANGO WA MUNGU Kifo ni matokeo ya dhambi, baada ya adamu na Hawa kuvunja sheria ya Mungu, pale kwenye bustani ya Edeni[mwanzo 3:1-24] Ikiwa Kama adamu na Hawa wasingetilia Shaka maagizo ya Mungu, Leo kifo kisingekuwepo kabisaa hakuna hata mmoja ambaye angekuwa anahisi maumivu tunayohisi leoo.... (EGW, Pendo lisilo kifani, sura ya Anguko la Mwanadamu) Biblia inafananisha KIFO na usingizi, maana baada ya muda Yesu akirudi...

UHALISIA WA UWEPO WA MUNGU

 JE MUNGU YUPO KWELI?  Watu wengi wamehoji maswali Mengi ikiwa Mungu yupo au la, na baadhi wamefikia hatua ya kusema kuwa hakuna Mungu!  Swali linakuja ikiwa Mungu yupo wawezaje kuthibitisha Imani yako?  UTHIBITISHO WA  UWEPO WA MUNGU  Mungu, yupo! Upo uthibitisho tosha kujibu swali hili Kama ifuatavyo!.  1. Uwepo wa Ulimwengu huu  Vitu vinavyoonekana vyote, Kama vile mimea, wanyama, mfumo wa jua (Solar system) na sayari zingine zote, kuwepo kwake Lazima awepo mwasisi wake! Maana hakuna uthibitisho wowote unaonesha kuwa sayari yaweza jiumba yenyewe!!, Wala dhana ya uibukaji haileti mantiki kusema mfumo wa Jua ulivyokaa uliibuka tuu.  2.  Mpangilio, mwafaka na Muundo wa Ulimwengu.  Jinsi Ulimwengu ulivyo, Kuna aliyepangilia, aka design(Muundo) ili kupata rangi/mwonekano mzuri wenye kuvutia, angalia aina za mimea, maua, wanyama tofauti kwa aina zake, ndege tofauti wakivutia sana!  Jua litoke mashariki kwenda magharibi Bila kuhama...

SIKU YA SABATO NI IPI?

Wengi, wanatunza Siku ya jumapili na wengine Siku ya jumamosi... Swali linakuja je, Kati ya hizi mbili ipi ni Siku ya kweli?...  SABATO YA BWANA  Biblia inasema;  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. [Waefeso 4:5] Kwa mujibu wa Biblia upo ubatizo mmoja(wa maji Mengi) Yuko Mungu mmoja na Imani moja.....(Siku ya ibada lazima iwe moja) Kama wakiwa na Imani moja....  SABATO NI AMRI YA NNE Katika kutoka 20:8-11 tunasoma maneno haya;  [8]Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.  [9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;  [10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.  [11]Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.  -----------------------------...