HUZUNI ILIJAZA MBINGU
Huzuni iliijaza mbingu, pale wote walipotambua kuwa wanadamu walikuwa wamepotea na dunia ambayo Mungu alikuwa ameiumba ilikuwa ijazwe na wanadamu wapatikanao na mauti wanaopitia maisha ya taabu, maradhi, na mauti, pasipo na njia ya kuokoka kwa mkosaji. Familia yote ya Adamu ni lazima wafe. - EGW, PLK 26.1
MPANGO WA KUMKOMBOA MWANADAMU
Ndipo Yesu akawafahamisha jeshi la malaika kwamba njia ya kuokoka ilikwisha kupatikana kwa ajili ya wanadamu waliopotea. - EGW, PLK 26.2
Aliwaambia kuwa alikuwa amemsihi Baba yake kwamba Yesu ajitolee maisha yake kuwa fidia ya kuwakomboa - EGW, PLK 26.2
Angetumikia adhabu ya kifo juu yake mwenyewe, ili kwa kupitia kwake wanadamu waweze kupata msamaha. - EGW,PLK 26.2
YESU KATIKA UMBO LA BINADAMU
Angeacha utukufu wake wote mbinguni, na kutokea duniani kama mwanadamu, kujinyenyekesha kama mwanadamu, kupitia uzoefu wake mwenyewe ajue majaribu mbalimbali ambayo yangewapata wanadamu, ili apate kujua jinsi ya kuwasaidia wale ambao wangejaribiwa - EGW, PLK 26.3, [Filipi 2:5-8]
Baada ya Mpango kuwekwa Yesu aliamua kuja duniani, kupitia tumbo la bikira mariam, akazaliwa Kama mtoto mchanga, akiisha kukua alianza kuhubiri neno la uzima [Mathayo 1:18-23]
KIFO CHA YESU MSALABANI
Hatimaye, baada ya kazi yake kama mwalimu kukamilishwa, angekabidhiwa katika mikono ya watu waovu na kustahimili karibu kila aina ya ukatili na maumivu ambayo Shetani pamoja na malaika zake wangeweza kuwachochea watu waovu kutenda - EGW, PLK 26.3
Mnamo mwaka wa 31 AD Siku ya ijumaa, Yesu alisulubishwa msalabani na Ijumaa jion, alizikwa kaburini, Kisha ilipofika jumapili Asubuhi alifufuka! [Luka 23:52-56, Luka 24:1-6]
KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA
Mwanadamu alipovunja Sheria ya Mungu (SoMo: ANGUKO LA MWANADAMU) ilikuwa afe milele, Yesu akatoa fidia, akafa badala yake mwanadamu, hivyo kupitia kwake Yesu uzima wa milele unapatikana, nafasi iliyokuwa imepotezwa Imerejea tena!!
Soma [Isaya 53:1-12].
Unataka kuiona Mbingu? Imekupasa kumwamini YESU Kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako,Kisha jitoe kwake, maana alikufa kwa ajili yako--
============================
Biblia inasema:
Yohana 3:16
Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
============================
Bwana kwa upendo wake, ametupatia nafasi ya pili, na iwapo hii Itapuuza haitakuwepo nafasi nyingine Tena!!
Je, tutaipuuza nafasi hii Tena, ambayo imegharimu maisha ya mwokozi aliyekubali kufa kwa ajili yangu na wewe??
-------------------
----Amani ya Bwana iwe Juu yako--. Hesabu 6:25
Comments
Post a Comment