Skip to main content

UZOEFU WA WOKOVU

Uzoefu wa wokovu hujumuisha kutubu, kuungama, msamaha, kuhesabiwa haki na kutakaswa. 

Mchakato huu huanza baada ya mwanadamu aliyeanguka dhambini kusikia wito ndani yake, ambao kimsingi ni sauti ya Roho mtakatifu inayonong'ona ndani yake, hivyo huanza kutambua dhambi yake na kuijutia.... ikiwa atakubali wito huo, hufanya uamuzi wa kufata hatua hizi, kutubu, kuungama , msamaha, kuhesabiwa haki na hatimaye hupata utakaso!![Matendo 2:37-38] 

1.KUTUBU(TOBA) 

Neno *kutubu / toba*, hutokana na neno la Kiebrania *nachum* lenye maana ya kuhuzunika, kusikitika. 

Neno la Kigiriki lenye maana sawa na hilo ni *metanoeo*, lenye maaana ya kubadilisha mawazo/nia-

Hivyo, aliyetenda dhambi baada ya kutambua dhambi yake, husikitika kwa kufanya hivyo, Kisha hunuia kuiacha! Na kubadilisha mwelekeo wake! Huku ndiko kutubu!! 

2. KUUNGAMA 

Kuungama ni kukiri au kukubali Jambo wazi wazi Bila kusema uongo! 
Aliyetenda dhambi baada ya kugundua kosa lake, hatua ya pili ni kuungama kwa Mungu, kuungama kwa mwanadamu mwenzakoo ni makosa, kwani naye pia ni mdhambi...[Mathayo 6:6] 
Biblia inasema: 
Isaya 1:18
Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu. 
---------------------- 
Bwana ni mwaminifu hata Kama dhambi zetu ni nyingi kiasi gani, tukiungama kwa dhati tutasamehewa!! 


3.KUHESABIWA HAKI 

Baada ya kuungama utapokea msamaha, baada ya kupokea msamaha, Bwana atakuhesabia haki kupitia kwake Yesu. 
Utahesabiwa kuwa huna hatia Tena!...sio kwa sababu ya matendo yako, Ila kwa kumwamini YESU na kutegemea haki yake, huku ukikiri kutostahili kwako..[1 kor 5:21] 

Baada ya kuhesabiwa haki ya Yesu, matokeo yake ni Kama ifuatavyo: 

A) Utakaso

Neno kutakaswa humaanisha kufanywa mtakatifu.
Toba ya kweli na kuhesabiwa haki huongoza kwenye kutakaswa, utakaso nayo ni kazi ya neema ya Mungu.
Hatua tatu za kutakaswa zinazofundishwa na Biblia ni: 
(i) ni jambo lililokwisha kutimizwa 
(ii) ni jambo linaloendelea kutimizwa sasa katika maisha ya mkristo 
(iii) ni jambo litakalokamilishwa Yesu akirudi Mara ya pili. 
Kwa wakati uliopita, wakati mtu anapohesabiwa haki, pia huwa amepokea utakaso kwa jina la Bwana Yesu [(1Kor. 6:11 cf. Yoh. 15:3)] 
Kama matokeo ya kuitwa na Mungu [Rum. 1:7] waumini huitwa watakatifu kwa kuwa wako katika Kristo [(Wafil. 1:1, Yoh. 15:1-7)] 


B) Kufanywa watoto wa Mungu.

Wakati huo huo tunapokea Roho ya kufanywa wana na warithi pamoja na Yesu [Rum. 8:15-17] Ni fursa bora kiasi gani, raha iliyoje?

C)Kuthibitishiwa wokovu.

Kuhesabiwa haki kunatuthibitishia kuwa ukombozi wetu ni hakika [Efe. 1:7]

D)Mwanzo wa maisha mapya ya ushindi. 

Maisha yake aliyetaswa yanakuwa tofauti kabisa, na ya Mwanzo maana tabia na makando kando yote yameachwa!! Ndani yake hujaa furaha, huku akingojea ahadi ya mwokozi wake!. 

E)Zawadi ya Uzima wa Milele.

Mahusiano yetu mapya na Yesu hutupatia zawadi ya uzima wa milele. Aliye na mwana ana uzima wa milele, asiye na mwana hana uzima [1Yoh. 5:12]

----------- 

Baada ya kuishi maisha ya ushindi, washindi watazawadiwa taji ya uzima, watarithi nchi mpya, na kupewa maisha yasio na dhambi Tena, ni furaha ajabu!! Tena isiyoelezeka kufika hapa!!....... 

====================

Barikiwa Sana, 

----Amani ya Bwana iwe Juu yako--- Hesabu6:25 

Comments

Popular posts from this blog

MTU ANAPOKUFA ANAENDA WAPI?

Mara nyingi, tumesikia hadithi nyingi kuhusu wafu, wengine wakiamini kuwa mtu anapokufa huwa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine, je! Ukweli halisi ni upi??  Karibu tujifunze pamojaa kwa kuangalia maandiko yanasemaje!!  MWANADAMU ALIUMBWA Mwanadamu ni matokeo ya udongo jumlisha pumzi ya uhai,  [Mwanadamu=udongo+pumzi ya uhai] BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo:2:7) Hivyo, ukichukua udongo ukatoa na pumzi ya uhai unapata maiti,  [Maiti=Udongo-pumzi ya uhai] KIFO HAUKUWA MPANGO WA MUNGU Kifo ni matokeo ya dhambi, baada ya adamu na Hawa kuvunja sheria ya Mungu, pale kwenye bustani ya Edeni[mwanzo 3:1-24] Ikiwa Kama adamu na Hawa wasingetilia Shaka maagizo ya Mungu, Leo kifo kisingekuwepo kabisaa hakuna hata mmoja ambaye angekuwa anahisi maumivu tunayohisi leoo.... (EGW, Pendo lisilo kifani, sura ya Anguko la Mwanadamu) Biblia inafananisha KIFO na usingizi, maana baada ya muda Yesu akirudi...

UHALISIA WA UWEPO WA MUNGU

 JE MUNGU YUPO KWELI?  Watu wengi wamehoji maswali Mengi ikiwa Mungu yupo au la, na baadhi wamefikia hatua ya kusema kuwa hakuna Mungu!  Swali linakuja ikiwa Mungu yupo wawezaje kuthibitisha Imani yako?  UTHIBITISHO WA  UWEPO WA MUNGU  Mungu, yupo! Upo uthibitisho tosha kujibu swali hili Kama ifuatavyo!.  1. Uwepo wa Ulimwengu huu  Vitu vinavyoonekana vyote, Kama vile mimea, wanyama, mfumo wa jua (Solar system) na sayari zingine zote, kuwepo kwake Lazima awepo mwasisi wake! Maana hakuna uthibitisho wowote unaonesha kuwa sayari yaweza jiumba yenyewe!!, Wala dhana ya uibukaji haileti mantiki kusema mfumo wa Jua ulivyokaa uliibuka tuu.  2.  Mpangilio, mwafaka na Muundo wa Ulimwengu.  Jinsi Ulimwengu ulivyo, Kuna aliyepangilia, aka design(Muundo) ili kupata rangi/mwonekano mzuri wenye kuvutia, angalia aina za mimea, maua, wanyama tofauti kwa aina zake, ndege tofauti wakivutia sana!  Jua litoke mashariki kwenda magharibi Bila kuhama...

SIKU YA SABATO NI IPI?

Wengi, wanatunza Siku ya jumapili na wengine Siku ya jumamosi... Swali linakuja je, Kati ya hizi mbili ipi ni Siku ya kweli?...  SABATO YA BWANA  Biblia inasema;  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. [Waefeso 4:5] Kwa mujibu wa Biblia upo ubatizo mmoja(wa maji Mengi) Yuko Mungu mmoja na Imani moja.....(Siku ya ibada lazima iwe moja) Kama wakiwa na Imani moja....  SABATO NI AMRI YA NNE Katika kutoka 20:8-11 tunasoma maneno haya;  [8]Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.  [9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;  [10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.  [11]Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.  -----------------------------...