Skip to main content

SHERIA YA MUNGU

 Kutoka mlima Sinai, Bwana mwenyewe aliandika sheria yake kwa Chanda chake mwenyewe.... Akiisha kuiandika alimkabidhi mtumishi wake Mussa, kupitia Sheria yake twaweza kuwa salamaa, kupitia Yesu atutegemezaye na kutupatia nguvu za kuenenda Kama sheria ilivyo!! [Kutoka 31:18]

-----------------

JE, UNAMPENDA MUNGU? 

Maandiko yanasema:

Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. 1Yohana 2:4. 

-- Sheria ya Mungu, ni maelekezo namna ya kuishi kwa yule aliyekombolewa kutoka kwenye utumwa wa dhambi....... Iwapo mtu huyo ataishi kinyume na maagizo hayo, ni dhahiri kuwa bado hajakombolewa, pili bado Hana utii kwa Bwana wake!... 

AMRI KUMI ZA MUNGU

Amri kumi za MUNGU tunazipata katika kitabu Cha kutoka 20:1-17 
............. 
Ziko katika mafungu mawili, ambayo ni 

A)Amri ya 1-4 zinahusu upendo Kati ya mwanadamu na Mungu 

B)Amri ya 5-10 zinahusu upendo Kati ya mwanadamu na mwanadamu mwenzake

1. AMRI YA KWANZA 

*[3]Usiwe na miungu mingine ila mimi*

2. AMRI YA PILI

[4]*Usijifanyie sanamu ya kuchonga*, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

[5]Usivisujudie wala kuvitumikia....... 

3. AMRI YA TATU 

*[7]Usilitaje bure jina la BWANA, Mungu wako,* maana BWANA hatamhesabia kuwa hana hatia mtu alitajaye jina lake bure. 

--- kuapa, kulitumia mahakami kuthibitisha uongo... hapana!! Usilitumie kufanya uongo uonekane kuwa ni ukweli... 

4. AMRI YA NNE 

[8] *Ikumbuke siku ya Sabato uitakase* 

[9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote

[10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako..........

5. AMRI YA TANO 

*[12]Waheshimu baba yako na mama yako*; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako

6. AMRI YA SITA 

*Usiue* 

7. AMRI YA SABA 

*[14]Usizini*

8. AMRI YA NANE 

*[15]Usiibe*

9. AMRI YA TISA 

*[16]Usimshuhudie jirani yako uongo*

10. AMRI YA KUMI 

[17]Usiitamani nyumba ya jirani yako, usimtamani mke wa jirani yako; wala mtumwa wake, wala mjakazi wake, wala ng’ombe wake, wala punda wake, wala cho chote alicho nacho jirani yako>> [kutoka 20:1-17] 

=========================

Sheria ya Mungu, haikuishia  msalabani, sheria ya Mungu itadumu milele;[math 5:17-18] 

Maana dhambi ilikuja kwa sababu ya kuvunja sheria, ukiondoa sheria hakuna dhambi tena, je, NI kweli hakuna dhambi...hapana, 

<<<<<Mkinipenda, mtazishika amri zangu..[Yoh 14:15]>>>>>> 

...........................................

Amani ya Bwana iwe Juu yako---Hesabu 6:25 

Comments

Popular posts from this blog

MTU ANAPOKUFA ANAENDA WAPI?

Mara nyingi, tumesikia hadithi nyingi kuhusu wafu, wengine wakiamini kuwa mtu anapokufa huwa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine, je! Ukweli halisi ni upi??  Karibu tujifunze pamojaa kwa kuangalia maandiko yanasemaje!!  MWANADAMU ALIUMBWA Mwanadamu ni matokeo ya udongo jumlisha pumzi ya uhai,  [Mwanadamu=udongo+pumzi ya uhai] BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo:2:7) Hivyo, ukichukua udongo ukatoa na pumzi ya uhai unapata maiti,  [Maiti=Udongo-pumzi ya uhai] KIFO HAUKUWA MPANGO WA MUNGU Kifo ni matokeo ya dhambi, baada ya adamu na Hawa kuvunja sheria ya Mungu, pale kwenye bustani ya Edeni[mwanzo 3:1-24] Ikiwa Kama adamu na Hawa wasingetilia Shaka maagizo ya Mungu, Leo kifo kisingekuwepo kabisaa hakuna hata mmoja ambaye angekuwa anahisi maumivu tunayohisi leoo.... (EGW, Pendo lisilo kifani, sura ya Anguko la Mwanadamu) Biblia inafananisha KIFO na usingizi, maana baada ya muda Yesu akirudi...

UHALISIA WA UWEPO WA MUNGU

 JE MUNGU YUPO KWELI?  Watu wengi wamehoji maswali Mengi ikiwa Mungu yupo au la, na baadhi wamefikia hatua ya kusema kuwa hakuna Mungu!  Swali linakuja ikiwa Mungu yupo wawezaje kuthibitisha Imani yako?  UTHIBITISHO WA  UWEPO WA MUNGU  Mungu, yupo! Upo uthibitisho tosha kujibu swali hili Kama ifuatavyo!.  1. Uwepo wa Ulimwengu huu  Vitu vinavyoonekana vyote, Kama vile mimea, wanyama, mfumo wa jua (Solar system) na sayari zingine zote, kuwepo kwake Lazima awepo mwasisi wake! Maana hakuna uthibitisho wowote unaonesha kuwa sayari yaweza jiumba yenyewe!!, Wala dhana ya uibukaji haileti mantiki kusema mfumo wa Jua ulivyokaa uliibuka tuu.  2.  Mpangilio, mwafaka na Muundo wa Ulimwengu.  Jinsi Ulimwengu ulivyo, Kuna aliyepangilia, aka design(Muundo) ili kupata rangi/mwonekano mzuri wenye kuvutia, angalia aina za mimea, maua, wanyama tofauti kwa aina zake, ndege tofauti wakivutia sana!  Jua litoke mashariki kwenda magharibi Bila kuhama...

SIKU YA SABATO NI IPI?

Wengi, wanatunza Siku ya jumapili na wengine Siku ya jumamosi... Swali linakuja je, Kati ya hizi mbili ipi ni Siku ya kweli?...  SABATO YA BWANA  Biblia inasema;  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. [Waefeso 4:5] Kwa mujibu wa Biblia upo ubatizo mmoja(wa maji Mengi) Yuko Mungu mmoja na Imani moja.....(Siku ya ibada lazima iwe moja) Kama wakiwa na Imani moja....  SABATO NI AMRI YA NNE Katika kutoka 20:8-11 tunasoma maneno haya;  [8]Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.  [9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;  [10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.  [11]Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.  -----------------------------...