Wengi, wanatunza Siku ya jumapili na wengine Siku ya jumamosi... Swali linakuja je, Kati ya hizi mbili ipi ni Siku ya kweli?...
SABATO YA BWANA
Biblia inasema;
Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
[Waefeso 4:5]
Kwa mujibu wa Biblia upo ubatizo mmoja(wa maji Mengi) Yuko Mungu mmoja na Imani moja.....(Siku ya ibada lazima iwe moja) Kama wakiwa na Imani moja....
SABATO NI AMRI YA NNE
Katika kutoka 20:8-11 tunasoma maneno haya;
[8]Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.
[9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;
[10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.
[11]Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.
---------------------------------
Hapa tunapata Mambo yafuatayo:
#Sabato itunzwe
#Sabato hutunzwa Siku ya Saba ya juma
#Sabato ni ya Bwana
#Sabato imetakaswa, imebarikiwa,
#Baada ya uumbaji Bwana aliacha kazi na kupumzika Siku hiyo.
SABATO NI LINI LEO?
Neno "sabato", Ina maana ya pumziko(rest) Siku hiyo mwanadamu anapaswa kupumzika, asifanye kazi yoyote (kutoka 20:10) Ila isipokuwa ibada tuu... ni Siku ya kufakari Mambo ya Mungu.
Kutoka 20:10 inasema sabato ni Siku ya Saba...swali je, hiyo Siku ya Saba ni lini kwenye Siku zetu hizi leo??
=====
Biblia inasema:
Luka 24:1-3
[1]Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari.
[2]Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi,
[3]Wakaingia, wasiuone mwili wa Bwana Yesu
Kwa mujibu wa Biblia Yesu alifufuka Siku ya 1 ya juma, ambayo Leo ndo jumapili,
"Kama tukihesabia jumapili(Siku ya kwanza) aliyofufuka Yesu, jumatatu itakuwa Siku ya pili......"jumamosi" itakuwa Siku ya Saba"
Hivyo, kutoka 20 inasema Siku ya Saba ni sabato ya Bwana, akimanisha jumamosi ni sabato ya Bwana, hivyo! Siku ya jumamosi ndo Siku ya sabato-- ya Bwana.
Jumamosi mwanadamu imempasa kupumzika na kuacha kazi zake, na kuutafuta Uso wa Bwana maana ni Siku ya sabato-- ya Bwana.
MADHARA YA KUVUNJA SABATO
Biblia inasema:
Yakobo 2:10
Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.
Kwa mujibu wa maandiko, ukivunja Amri ya Nne(sabato) ni sawa na yule ambaye hashiki Amri za MUNGU.....hivyo, Hukumu yake ni sawa na ya yule afanyae wizi, uzinzi....na maovu mengine.
JE, SABATO ILIISHIA MSALABANI?
Kujibu swali hili, zingatia haya;
##Sabato itadumu milele, Isaya 66:22-23
##Yesu alitunza sabato, Luka 4:16
##Mitume walitunza Sabato, Matendo 16:13
##Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu Marko 2:27.
==================================================================================================================
Kwa hiyo, Sabato haikuishia msalabani,,,,maana hata baada ya Yesu kupaa mbinguni mitume waliendelea kuitunza!!
Karibu, SoMo lijalo...tutaangalia nini kilitokea Hadi leo wengi wanashika jumapili
ambayo sio agizo la Mungu kabisaa!
----Amani ya Bwana iwe juu yako Hesabu 6:24-----
Amen,
ReplyDeleteBe blessed by God
Amen....you too!!
DeleteKwaiyo hiki kitabu kipo kwanjia ya link tu peke yake au?
ReplyDeleteNitafute WhatsApp number 0752377430 nikutumie kitabu kabisaaa!
DeleteHapana, kipo Kama kitabu piaa!
ReplyDelete