Skip to main content

UHALISIA WA UWEPO WA MUNGU

 JE MUNGU YUPO KWELI? 

Watu wengi wamehoji maswali Mengi ikiwa Mungu yupo au la, na baadhi wamefikia hatua ya kusema kuwa hakuna Mungu! 

Swali linakuja ikiwa Mungu yupo wawezaje kuthibitisha Imani yako? 


UTHIBITISHO WA  UWEPO WA MUNGU 

Mungu, yupo! Upo uthibitisho tosha kujibu swali hili Kama ifuatavyo!. 

1. Uwepo wa Ulimwengu huu 

Vitu vinavyoonekana vyote, Kama vile mimea, wanyama, mfumo wa jua (Solar system) na sayari zingine zote, kuwepo kwake Lazima awepo mwasisi wake! Maana hakuna uthibitisho wowote unaonesha kuwa sayari yaweza jiumba yenyewe!!, Wala dhana ya uibukaji haileti mantiki kusema mfumo wa Jua ulivyokaa uliibuka tuu. 

2.  Mpangilio, mwafaka na Muundo wa Ulimwengu. 

Jinsi Ulimwengu ulivyo, Kuna aliyepangilia, aka design(Muundo) ili kupata rangi/mwonekano mzuri wenye kuvutia, angalia aina za mimea, maua, wanyama tofauti kwa aina zake, ndege tofauti wakivutia sana! 
Jua litoke mashariki kwenda magharibi Bila kuhama kwenye mzunguko wake! 
Uibukaji usingeweza kufanya hivi, maana vitu vilivyotenegenezwa na Binadamu vina kasoro, ila vya asili havina kasoro, hii ni kusema uibukaji/mlipuko unazidi akili Binadamu!! La, 
---Hapa lazima awepo aliyekuwa asimamia na kuratibu mambo yote haya!  

3. Sayansi ya uchunguzi ya jamii za wanadamu

Kila mwanadamu anajua jema na baya, hata wanyama pori pia wana Nidhamu Fulani ndani yao ya utii, walipewa na Nani,,,,,Hawa wanyama? 
Uwepo wa dhamiri ndani ya mwanadamu huonesha kuwa Yupo aliyeweka hiyo dhamiri,
Dhana ya kuibuka, haiwezi kutoa dhamiri ya kujua Mema na mabaya!! maana na yenyewe haijui chochote! 

4. Hulka ya Ufahamu 

 Kila mwanadamu kwa asili ana amini uwepo wa nguvu iliyo Juu ya uwezo wake, ndo maana kila jamii Wana mfumo wa ibada, utakuta anaabudu kitu Fulani.... 
--- Hii inaonesha uwepo dhahiri wa nguvu(Mungu) iliyo chimbuko letu!   

5. Uthibitisho wa maandiko

Kwa kuangalia Biblia inafunua kuwa Mungu yupo, na ndiye Muumbaji wa vyote vilivyoko duniani.
Katika mwanzo sura ya 01 yote. 

6. Mizani ya nguvu za kiroho  

Tumeshuhudia mapepo yakitolewa!! Kwa maombi tu, Miujiza! Iliyo kinyume na nguvu za Giza,  uwezo wa kufufua mtu kwa ombi tu,  
Miujiza yote hiyo huashiria utendaji kazi wa nguvu  kubwa zaidi(Mungu) 
---Daima halikushindikana Jambo lolote Alipoitwa huyu muumbaji kwa dhati, hii huonesha kuwa yupo ndo maana anajibu maombi.  
.................................

---Amani ya Bwana iwe Juu yako----                     Hesabu 6:25 

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

MTU ANAPOKUFA ANAENDA WAPI?

Mara nyingi, tumesikia hadithi nyingi kuhusu wafu, wengine wakiamini kuwa mtu anapokufa huwa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine, je! Ukweli halisi ni upi??  Karibu tujifunze pamojaa kwa kuangalia maandiko yanasemaje!!  MWANADAMU ALIUMBWA Mwanadamu ni matokeo ya udongo jumlisha pumzi ya uhai,  [Mwanadamu=udongo+pumzi ya uhai] BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo:2:7) Hivyo, ukichukua udongo ukatoa na pumzi ya uhai unapata maiti,  [Maiti=Udongo-pumzi ya uhai] KIFO HAUKUWA MPANGO WA MUNGU Kifo ni matokeo ya dhambi, baada ya adamu na Hawa kuvunja sheria ya Mungu, pale kwenye bustani ya Edeni[mwanzo 3:1-24] Ikiwa Kama adamu na Hawa wasingetilia Shaka maagizo ya Mungu, Leo kifo kisingekuwepo kabisaa hakuna hata mmoja ambaye angekuwa anahisi maumivu tunayohisi leoo.... (EGW, Pendo lisilo kifani, sura ya Anguko la Mwanadamu) Biblia inafananisha KIFO na usingizi, maana baada ya muda Yesu akirudi...

SIKU YA SABATO NI IPI?

Wengi, wanatunza Siku ya jumapili na wengine Siku ya jumamosi... Swali linakuja je, Kati ya hizi mbili ipi ni Siku ya kweli?...  SABATO YA BWANA  Biblia inasema;  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. [Waefeso 4:5] Kwa mujibu wa Biblia upo ubatizo mmoja(wa maji Mengi) Yuko Mungu mmoja na Imani moja.....(Siku ya ibada lazima iwe moja) Kama wakiwa na Imani moja....  SABATO NI AMRI YA NNE Katika kutoka 20:8-11 tunasoma maneno haya;  [8]Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.  [9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;  [10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.  [11]Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.  -----------------------------...