Skip to main content

UUMBAJI

 UUMBAJI WA SAYARI YETU YA DUNIA 

Dunia yetu hii na vyote vilivyomo viliumbwa na Mungu kwa muda wa siku sita. Hapa ni siku sita za masaa 24HRS, (Yome[Hebrew]- inayotafasiliwa Kama siku...inamanisha tangu jua kuzama Hadi Jua kuzama sio miaka 6,000 Kama waanavyodhani wengine. [Mwanzo 1:1]

Dunia Ina vitu vingi, ndiyo! Mimea aina tofauti, wanyama, n.k kwa Mungu haya sio Mengi kiasi Cha kushindwa kuumba kwa Siku sita tuu,  alikuwa anatamka vinatokea!! Kama ifuatavyo; 


 -- Siku ya kwanza (01)

Siku ya kwanza Mungu aliumba *NURU*         hapo  ndipo mwanzo wa Giza na Nuru ulipopatikana..... 

Mwanzo 1:3-5
[3]Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru... 

-- Siku ya pili (02)

Siku ya pili Mungu aliumba *ANGA* 

Mwanzo 1:6-8 
[6 ]Mungua akasema Na liwe anga katikati ya maji, likayatenge maji na maji.... 

-- Siku ya tatu (03) 

Siku ya tatu Mungu aliumba, *NCHI KAVU* *BAHARI* na *MIMEA* 

Mwanzo 1:9-11
[9]Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane; ikawa hivyo. 

[10]Mungu akapaita pale pakavu nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. 

[11]Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo. 

-- Siku ya Nne (04) 

Siku ya Nne Mungu aliumba *JUA* *MWEZI* na *NYOTA* 

Mwanzo 1:14-19
[16]Mungu akafanya mianga miwili mikubwa, ule mkubwa utawale mchana, na ule mdogo utawale usiku; akafanya na nyota pia. 

-- Siku ya tano (05) 

Siku ya tano Mungu aliumba *VIUMBE WA MAJINI* na *NDEGE WA ANGANI* 

Mwanzo 1:20-23 
[20]Mungu akasema, Maji na yajawe kwa wingi na kitu kiendacho chenye uhai, na ndege waruke juu ya nchi katika anga la mbingu. 

-- Siku ya Sita (06) 

Siku ya mwisho(06) Mungu aliumba *WANYAMA WOTE* na akamalizia kwa kumuumba *MWANADAMU* 

Mwanzo 1:24-31
[24]Mungu akasema, Nchi na izae kiumbe hai kwa jinsi zake, mnyama wa kufugwa, nacho kitambaacho, na wanyama wa mwitu kwa jinsi zake; ikawa hivyo. 

[26]Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. 
-------------------------------
-------------------------------

Binadamu Ndiye kiumbe pekee aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, 

Mwanadamu alipotoka mikononi mwa Mungu alikuwa mkamilifu, Bila dosari... Ndani yake akiwa na tabia halisi ya Mungu!! 

Kila kitu kilichoumbwa na MUNGU, kilikuwa chema! 
Mwanzo 1:31 
Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita... 
---------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
Leo, dunia imeharibika, ubora umepotea, dunia Imekuwa Tena haitamaniki, nini kilichotekea mpaka dunia Imekuwa hivi? 
----------------------------------
Endelea kufatilia, masomo yanayofuata tutajifunza!! Nini kilitokea! 

---- Amani ya Bwana iwe Juu yako----             Hesabu 6:25 















Comments

  1. Replies
    1. Alright, we thank you for good feedback, keep visiting our blog for more lessons!

      Delete

Post a Comment

Popular posts from this blog

MTU ANAPOKUFA ANAENDA WAPI?

Mara nyingi, tumesikia hadithi nyingi kuhusu wafu, wengine wakiamini kuwa mtu anapokufa huwa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine, je! Ukweli halisi ni upi??  Karibu tujifunze pamojaa kwa kuangalia maandiko yanasemaje!!  MWANADAMU ALIUMBWA Mwanadamu ni matokeo ya udongo jumlisha pumzi ya uhai,  [Mwanadamu=udongo+pumzi ya uhai] BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo:2:7) Hivyo, ukichukua udongo ukatoa na pumzi ya uhai unapata maiti,  [Maiti=Udongo-pumzi ya uhai] KIFO HAUKUWA MPANGO WA MUNGU Kifo ni matokeo ya dhambi, baada ya adamu na Hawa kuvunja sheria ya Mungu, pale kwenye bustani ya Edeni[mwanzo 3:1-24] Ikiwa Kama adamu na Hawa wasingetilia Shaka maagizo ya Mungu, Leo kifo kisingekuwepo kabisaa hakuna hata mmoja ambaye angekuwa anahisi maumivu tunayohisi leoo.... (EGW, Pendo lisilo kifani, sura ya Anguko la Mwanadamu) Biblia inafananisha KIFO na usingizi, maana baada ya muda Yesu akirudi...

UHALISIA WA UWEPO WA MUNGU

 JE MUNGU YUPO KWELI?  Watu wengi wamehoji maswali Mengi ikiwa Mungu yupo au la, na baadhi wamefikia hatua ya kusema kuwa hakuna Mungu!  Swali linakuja ikiwa Mungu yupo wawezaje kuthibitisha Imani yako?  UTHIBITISHO WA  UWEPO WA MUNGU  Mungu, yupo! Upo uthibitisho tosha kujibu swali hili Kama ifuatavyo!.  1. Uwepo wa Ulimwengu huu  Vitu vinavyoonekana vyote, Kama vile mimea, wanyama, mfumo wa jua (Solar system) na sayari zingine zote, kuwepo kwake Lazima awepo mwasisi wake! Maana hakuna uthibitisho wowote unaonesha kuwa sayari yaweza jiumba yenyewe!!, Wala dhana ya uibukaji haileti mantiki kusema mfumo wa Jua ulivyokaa uliibuka tuu.  2.  Mpangilio, mwafaka na Muundo wa Ulimwengu.  Jinsi Ulimwengu ulivyo, Kuna aliyepangilia, aka design(Muundo) ili kupata rangi/mwonekano mzuri wenye kuvutia, angalia aina za mimea, maua, wanyama tofauti kwa aina zake, ndege tofauti wakivutia sana!  Jua litoke mashariki kwenda magharibi Bila kuhama...

SIKU YA SABATO NI IPI?

Wengi, wanatunza Siku ya jumapili na wengine Siku ya jumamosi... Swali linakuja je, Kati ya hizi mbili ipi ni Siku ya kweli?...  SABATO YA BWANA  Biblia inasema;  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. [Waefeso 4:5] Kwa mujibu wa Biblia upo ubatizo mmoja(wa maji Mengi) Yuko Mungu mmoja na Imani moja.....(Siku ya ibada lazima iwe moja) Kama wakiwa na Imani moja....  SABATO NI AMRI YA NNE Katika kutoka 20:8-11 tunasoma maneno haya;  [8]Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.  [9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;  [10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.  [11]Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.  -----------------------------...