SoMo lililopita tuliona kuwa ukimwamini Yesu, ukatubu utasamehewa dhambi, hata Kama zilikuwa nyingi kiasi gani....upendo mkuu ajabu! Kiroho mtu aweza kuzaliwa Mara ya pili kwa njia ya ubatizo!...... Kwa njia ya ubatizo, mtu atamkiri Yesu, kuwa ni mwokozi wake, ndiyo njia Mungu aliyoiweka ya kutuvusha kutoka mahali pa dhambi, kutuunganisha na Mwokozi, kwa kufanya tendo hili...inakuwa umemkubali Yesu waziwazi.... hivyo, baada ya kubatizwa atakupokea, Kama mtoto wake!....nawe utakuwa umeanza safari mpya ya maisha! UBATIZO Je, mtu anayebatizwa anapaswa awe na sifa gani? Biblia inasema: Marko 16:15-16 [15]Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe. [16]Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa. Kutoka kwenye Aya hii tunapata Mambo 3. a) Injili Kabla mtu hajabatizwa lazima ajue kweli (Neno la Mungu), ili aelewe anabatizwa kwa sababu gani!. b)Imani Baada ya kuhubiriwa, na kuitikia sauti ya ...