Skip to main content

Posts

KWANINI WENGI WANASALI JUMAPILI?

 Hili limekuwa swali kuu, kwanini idadi kubwa ya watu wanashika Siku ya kwanza(01) ya juma yaani jumapili Kama Siku ya ibada?  Katika Somo la Siku ya sabato ni ipi tumejifunza, kuwa sabato ya kweli ni jumamos:  Ikiwa ndivyo, jumapili iliingiaje Kama Siku ya ibada, hadi wengi wanaishika leoo...karibu tujifunze pamoja....  *YESU ALITUNZA SABATO* Katika kitabu Cha Luka 4:16 anasema: ilikuwa desturi ya Mwokozi kusali Siku ya sabato(jumamosi) kumbe Yesu hakutunza jumapili Kama Siku ya ibada ....  *MITUME WALITUNZA SABATO*  Katika kitabu Cha matendo 16:13 neno linasema: Mitume hata baada ya Yesu kupaa mbinguni bado waliendelea kutunza sabato .....kamwe hawakushika jumapili, maana ilikuwa Siku ya kazi.  *BADILIKO LA SABATO, LILITABIRIWA KWENYE MAANDIKO Katika kitabu Cha Daniel 7:25 inasema: [25]Naye atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wa...
Recent posts

MTU ANAPOKUFA ANAENDA WAPI?

Mara nyingi, tumesikia hadithi nyingi kuhusu wafu, wengine wakiamini kuwa mtu anapokufa huwa anaendelea kuishi katika ulimwengu mwingine, je! Ukweli halisi ni upi??  Karibu tujifunze pamojaa kwa kuangalia maandiko yanasemaje!!  MWANADAMU ALIUMBWA Mwanadamu ni matokeo ya udongo jumlisha pumzi ya uhai,  [Mwanadamu=udongo+pumzi ya uhai] BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. (Mwanzo:2:7) Hivyo, ukichukua udongo ukatoa na pumzi ya uhai unapata maiti,  [Maiti=Udongo-pumzi ya uhai] KIFO HAUKUWA MPANGO WA MUNGU Kifo ni matokeo ya dhambi, baada ya adamu na Hawa kuvunja sheria ya Mungu, pale kwenye bustani ya Edeni[mwanzo 3:1-24] Ikiwa Kama adamu na Hawa wasingetilia Shaka maagizo ya Mungu, Leo kifo kisingekuwepo kabisaa hakuna hata mmoja ambaye angekuwa anahisi maumivu tunayohisi leoo.... (EGW, Pendo lisilo kifani, sura ya Anguko la Mwanadamu) Biblia inafananisha KIFO na usingizi, maana baada ya muda Yesu akirudi...

SIKU YA SABATO NI IPI?

Wengi, wanatunza Siku ya jumapili na wengine Siku ya jumamosi... Swali linakuja je, Kati ya hizi mbili ipi ni Siku ya kweli?...  SABATO YA BWANA  Biblia inasema;  Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja. [Waefeso 4:5] Kwa mujibu wa Biblia upo ubatizo mmoja(wa maji Mengi) Yuko Mungu mmoja na Imani moja.....(Siku ya ibada lazima iwe moja) Kama wakiwa na Imani moja....  SABATO NI AMRI YA NNE Katika kutoka 20:8-11 tunasoma maneno haya;  [8]Ikumbuke siku ya Sabato uitakase.  [9]Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote;  [10]lakini siku ya saba ni Sabato ya BWANA, Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yo yote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako.  [11]Maana, kwa siku sita BWANA alifanya mbingu, na nchi, na bahari, na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba; kwa hiyo BWANA akaibarikia siku ya Sabato akaitakasa.  -----------------------------...

SHERIA YA MUNGU

 Kutoka mlima Sinai, Bwana mwenyewe aliandika sheria yake kwa Chanda chake mwenyewe.... Akiisha kuiandika alimkabidhi mtumishi wake Mussa, kupitia Sheria yake twaweza kuwa salamaa, kupitia Yesu atutegemezaye na kutupatia nguvu za kuenenda Kama sheria ilivyo!! [Kutoka 31:18] ----------------- JE, UNAMPENDA MUNGU?  Maandiko yanasema: Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. 1Yohana 2:4.  -- Sheria ya Mungu, ni maelekezo namna ya kuishi kwa yule aliyekombolewa kutoka kwenye utumwa wa dhambi....... Iwapo mtu huyo ataishi kinyume na maagizo hayo, ni dhahiri kuwa bado hajakombolewa, pili bado Hana utii kwa Bwana wake!...  AMRI KUMI ZA MUNGU Amri kumi za MUNGU tunazipata katika kitabu Cha kutoka 20:1-17  .............  Ziko katika mafungu mawili, ambayo ni  A)Amri ya 1-4 zinahusu upendo Kati ya mwanadamu na Mungu  B)Amri ya 5-10 zinahusu upendo Kati ya mwanadamu na mwanadamu mwenzake 1. AMRI YA KWANZA...

KUZALIWA MARA YA PILI

SoMo lililopita tuliona kuwa ukimwamini Yesu, ukatubu utasamehewa dhambi, hata Kama zilikuwa nyingi kiasi gani....upendo mkuu ajabu! Kiroho mtu aweza kuzaliwa Mara ya pili kwa njia ya ubatizo!......  Kwa njia ya ubatizo, mtu atamkiri Yesu, kuwa ni mwokozi wake, ndiyo njia Mungu aliyoiweka ya kutuvusha kutoka mahali pa dhambi, kutuunganisha na Mwokozi, kwa kufanya tendo hili...inakuwa umemkubali Yesu waziwazi.... hivyo, baada ya kubatizwa atakupokea, Kama mtoto wake!....nawe utakuwa umeanza safari mpya ya maisha!  UBATIZO Je, mtu anayebatizwa anapaswa awe na sifa gani?  Biblia inasema:  Marko 16:15-16 [15]Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.  [16]Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa.  Kutoka kwenye Aya hii tunapata Mambo 3.  a) Injili  Kabla mtu hajabatizwa lazima ajue kweli (Neno la Mungu), ili aelewe anabatizwa kwa sababu gani!.  b)Imani  Baada ya kuhubiriwa, na kuitikia sauti ya ...

UZOEFU WA WOKOVU

Uzoefu wa wokovu hujumuisha kutubu, kuungama, msamaha, kuhesabiwa haki na kutakaswa.  Mchakato huu huanza baada ya mwanadamu aliyeanguka dhambini kusikia wito ndani yake, ambao kimsingi ni sauti ya Roho mtakatifu inayonong'ona ndani yake, hivyo huanza kutambua dhambi yake na kuijutia.... ikiwa atakubali wito huo, hufanya uamuzi wa kufata hatua hizi, kutubu, kuungama , msamaha, kuhesabiwa haki na hatimaye hupata utakaso!![Matendo 2:37-38]  1.KUTUBU(TOBA)  Neno *kutubu / toba*, hutokana na neno la Kiebrania *nachum* lenye maana ya kuhuzunika, kusikitika.  Neno la Kigiriki lenye maana sawa na hilo ni *metanoeo*, lenye maaana ya kubadilisha mawazo/nia- Hivyo, aliyetenda dhambi baada ya kutambua dhambi yake, husikitika kwa kufanya hivyo, Kisha hunuia kuiacha! Na kubadilisha mwelekeo wake! Huku ndiko kutubu!!  2. KUUNGAMA  Kuungama ni kukiri au kukubali Jambo wazi wazi Bila kusema uongo!  Aliyetenda dhambi baada ya kugundua kosa lake, hatua ya pili ni kuunga...

SULUHISHO BAADA YA ANGUKO

 HUZUNI ILIJAZA MBINGU Huzuni iliijaza mbingu, pale wote walipotambua kuwa wanadamu walikuwa wamepotea na dunia ambayo Mungu alikuwa ameiumba ilikuwa ijazwe na wanadamu wapatikanao na mauti wanaopitia maisha ya taabu, maradhi, na mauti, pasipo na njia ya kuokoka kwa mkosaji. Familia yote ya Adamu ni lazima wafe. - EGW, PLK 26.1 MPANGO WA KUMKOMBOA MWANADAMU  Ndipo Yesu akawafahamisha jeshi la malaika kwamba njia ya kuokoka ilikwisha kupatikana kwa ajili ya wanadamu waliopotea. - EGW, PLK 26.2 Aliwaambia kuwa alikuwa amemsihi Baba yake kwamba Yesu ajitolee maisha yake kuwa fidia ya kuwakomboa - EGW, PLK 26.2 Angetumikia adhabu ya kifo juu yake mwenyewe, ili kwa kupitia kwake wanadamu waweze kupata msamaha. -  EGW,PLK 26.2 YESU KATIKA UMBO LA BINADAMU Angeacha utukufu wake wote mbinguni, na kutokea duniani kama mwanadamu, kujinyenyekesha kama mwanadamu, kupitia uzoefu wake mwenyewe ajue majaribu mbalimbali ambayo yangewapata wanadamu, ili apate kujua jinsi ya kuwasaidia w...